Posts

Trump awasili Saudi Arabia

Image
Rais Donald Trump  akikaribishwa  kwa bashasha  kubwa  na  ukoo  wa  kifalme  wa  Saudi Arabia  jana , wakati  akiweka  kando, japokuwa  kwa  muda  tu , utata mkubwa  unaoukumba utawala  wake  mjini  Washington. Rais Trump akilakiwa mjini Riyadh Trump  amewazawadia  wenyeji wake  mpango  wa mauzo  ya  bilioni 110  wa  silaha  wenye  lengo  la  kuimarisha  usalama  wa  Saudi  Arabia pamoja  na  makubaliano  kadhaa  ya  kibishara. "Hii  ni  siku  muhimu  sana, uwekezaji  mkubwa  katika  Marekani ," Trump  alisema wakati wa  mkutano  na  mwanamfalme Mohammed bin Nayef. Rais Trump (Kushoto) akisalimiana na mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz(kulia) Ziara  katika  mji  mkuu  wa  Saudi Arabia  iliku...

Polisi waua watatu wanaodaiwa majambazi Mwanza

Image
Polisi mkoani Mwanza wamewaua watuhumiwa watatu wa ujambazi baada ya majibizano ya risasi kati yao na askari wa jeshi la polisi huku wengine watatu wakikimbia. Polisi pia wamefanikiwa kukamata bunduki aina ya ‘shotgun’ na magazine mbili zikiwa na risasi mbili na maganda mawili. Kaimu kamishna wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amewataja waliouwawa leo (Ijumaa) kuwa ni Benedict Tobias, Mabula Segeja na Charles Thomas huku wenzao watatu wakikimbia. “Askari walipowabaini majimbazi hao katika eneo ambalo walipanga kukutana waliawataka kujisalimisha lakini majambazi hao walikaidi na kuanza kurusha risasi ambayo ili mjeruhi mwenzao ndipo askari nao wakaanza kujibu ,”amesema Msangi. Amesema miili ya watuhumiwa hao wa ujambazi imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa Bugando kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi. Kamanda huyo amesema  msako wa kuwatafuta waliokimbia bado unaendelea.